BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, January 22, 2010

FADDY DADDY MKALI WA BONGO FLAVA KUTOKEA TANGA CITY!

Msanii kutoka mkoani Tanga Faddy Dady, akiwa katika Pozz punde baada ya kufanya Interview kwenye kipindi cha The Hot Beat kinachorushwa na Mwambao Fm Radio hapa jijini Tanga. Faddy ambaye amewahi kutamba na wimbo wa "Moyoni Naumia" ambao ulimtambulisha vizuri kunako game ya muziki wa Bongo Flava.

Hapa akiwa na Dj Roja Kiss wa Mwambao Fm. Faddy sasa anatamba na ngoma yake kali ya "Asali Shubiri" aliyoirekodi kwa producer Steve White chini ya studio Land Line Production.

(Akiwa na Dj Roja Kiss na Dj Bob Nass wa Breeze Fm Radio) Mchizi hivi sasa yupo chuo pale mlimani anapiga buku na ametanabaisha kuwa albamu yake ya "NIMEUPATA VIPI" ipo sokoni kwa hiyo unaweza kujipatia copy yako. Faddy amemalizia kuwa anatarajia kuachia singo yake ya tatu wiki ijayo ambayo ameifanya pale Akinato Record chini ya producer lil Gheto.







No comments:

Post a Comment