BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Friday, January 29, 2010

DAZ BABA KWISHAAAA!! ATUMIKISHWA HOVYO

Ni habari ya kusikitisha sana kwa msanii aliyewahi kuwa mkubwa kama Daz Baba kusikia habari kama hii.

Kutoka chanzo kimoja chini ya kapeti inasemakana Daz Baba ni kama Houseboy wa P Funk Majani pale studio za Bongo Record, kwani kila kitu hata sigara dukani jamaa hutumwa.

“E bwana utamuhurumia sana Daz, siku nzima anashinda pale studio kwa Majani na kila kitu anatumwa yeye hata kusafisha studio pale anasafisha yeye, yani Daz anasikitisha sana, dukani yeye, kuleta hata maji ya kunywa ni yeye” kilisema chanzo hicho

Jamaa alizidi kuongeza “yani anaweza kupita mara kumi hapa anaenda na kurudi dukani kama kitololi vile.” alimaliza

Daz Baba ni mmoja wa wanamuziki wa lile kundi lililotamba sana miaka ya nyuma Daz Nundaz ambalo alikuwepo yeye, Ferouz, Sajo, La Rhumba na wengine.

VIJIMAMBO VYA TANGA ilijaribu kwa kila hali na mali kumtafuta Daz Baba athibitishe hilo lakini simu yake ilikuwa haipatikani.







No comments:

Post a Comment